Wasomi watoa maoni kuhusu EPA
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, akisalimiana na Profesa Helmut Asche ambaye ni mtaalam wa masuala ya uchumi, sayansi ya jamii na mtangamano wa kikanda mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Cive, Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Profesa Asche ambaye ni raia wa Ujerumani amefanya mudhara wa umma kuhusu manufaa na chagamoto za Mkataba wa Ubia wa Kiuchumi (Economic Partnership Agreement -EPA) baina ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Umoja wa Ulaya (EAC).
Profesa Helmut Asche akiwasilisha mada hiyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt Faraji Kasidi Mnyepe (wa kwanza kushoto) akifuatilia mada hiyo. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Edwin Mhede.
Mmoja kati ya washiriki wa mkutano huo akiuliza swali.