Rais Ramaphosa aitembelea kambi ya Wapigania uhuru wa Afrika Kusini iliyopo Mazimbu, Morogoro
Rais Ramaphosa aitembelea kambi ya Wapigania uhuru wa Afrika Kusini iliyopo Mazimbu, Morogoro
Mhe. Prof. Kabudi naye akizungumza wakati wa ziara ya Rais wa Afrika Kusini mkoani Morogoro
Mhe. Rais Ramaphosa akizungumza wakati alipotembelea kambi za wapigaia uhuru kutoka Afrika Kusini zilizopo Mazimbu mkoani Morogoro. Katika hotuba yake alitoa shukrani kwa Watanzania hususan wakazi wa eneo hilo kwa mchango mkubwa walioutoa ikiwemo kutoa eneo na kuwahifadhi wapigania uhuru wa nchi hiyo ambapo alisema amefarijika kukanyaga ardhi hiyo yenye historia kubwa ya ushirikiano wa kindugu kati ya Tanzania na Afrika Kusini. Pia aliahidi kuhakikisha nchi yake inaimarisha soko la mazao mbalimbali kutoka Morogoro na pia kuifanya kambi hiyo kuwa kituo kikubwa cha utalii.