Prof. Kabudi apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule nchini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akipokea nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa India, Mhe. Sanjiv Kohli. Hafla hiyo ilifanyika katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.