Balozi Mteule wa Umoja wa Falme za Kiarabu awasilisha Nakala za Hati za Utambulisho
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), amepokea nakala za hati za utambulisho za Balozi Mteule wa Umoja wa Falme za Kiarabu nchini Tanzania Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohammed Al Marzooqi, tukio hilo limefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar es Salaam tarehe 29 Octoba, 2018.