Skip to main content
News and Events

BALOZI MBAROUK AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUMUAGA BALOZI EDWIN RUTAGERUKA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) akiongoza waombolezaji katika kuaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasi ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Marehemu Balozi Edwin Rutageruka katika kijiji cha Musibuka, Wilayani Misenyi Mkoani Kagera.

  • Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) akitoa salamu za mwisho kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasi ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Marehemu Balozi Edwin Rutageruka katika mazishi yaliyofanyika kijiji cha Musibuka, Wilayani Misenyi Mkoani Kagera
  • Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akitoa salamu za rambirambi kwa ndugu na jamaa wa familia ya marehemu Balozi Edwin Rutageruka wakati wa mazishi yaliyofanyika katika kijiji cha Musibuka Wilayani Misenyi Mkoani Kagera
  • Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) pamoja na mume wake wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Balozi Edwin Rutageruka
  • Naibu Waziri Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara wakiwa katika picha ya pamoja kwenye kaburi la Marehemu Balozi Edwin Rutageruka mara baada ya maziko ya Balozi Edwin Rutegaruka