VIONGOZI WAKUU WA NCHI NA SERIKALI DUNIANI WASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA JPM
Rais wa Ethiopia Mhe. Sahle-Work Zewde akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
Naibu Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Ulinzi wa Serikali ya Oman, Mtukufu Sayyid Shihab bin Tarik bin Taimur Al-Said, akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli