Skip to main content
News and Events

BALOZI MBAROUK AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI WA KAMPUNI YA SHELL

BALOZI MBAROUK AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI WA KAMPUNI YA SHELL

Mheshimiwa Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo tarehe 3 Juni 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Bw. Ahmed Salim anayeratibu Mahusiano kati ya Kampuni ya Shell na Serikali. Bw. Salim ameeleza ameeleza lengo la ziara yake Wizarani ni kuelezea dhamira ya Kampuni ya Shell ya kuwekeza katika Sekta ya Gesi (LNG) Nchini. 

Balozi Mbarouk licha ya kupongeza uamuzi wa Kampuni ya Shell ya kuwekeza nchini amemweleza Bw. Salim kuwa Wizara na Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano kwa kampuni hiyo katika shughuli zao uwekezaji. Pia amweleza kuhusu dhamira ya Serikali ya kuendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na ufanyaji biashara nchini. 

Bw. Salim ameeleza kuwa Kampuni ya Shell inatarajia kufanya uwekezaji wenye thamini ya fedha za kitanzania zaidi shilingi bilioni 30.

 

  • Mazungumzo yakiendelea
  • Mheshimiwa Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akimkaribisha Bw. Ahmed Salim anayeratibu Mahusiano kati ya Kampuni ya Shell na Serikali alipowasili Wizarani jijini Dodoma.
  • Mheshimiwa Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akimsikiliza Bw. Ahmed Salim anayeratibu Mahusiano kati ya Kampuni ya Shell na Serikali alipowasili Wizarani jijini Dodom
Downloads File: