Skip to main content
News and Events

WAZIRI MULAMULA AFUNGUA MKUTANO WA WANAWAKE KATIKA DIPLOMASIA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) leo tarehe 23 Machi 2022 amefungua mkutano wa Wanawake katika Diplomasia (Women in Diplomacy) unaofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.


Akizungumza wakati anafungua mkutano huo Waziri Mulamula amehimiza umuhimu wa kutumia Diplomasia katika kuleta amani na maridhiano katika jamii. “Ujumbe wangu kwenu katika siku hii muhimu ni kuwa, Diplomasia itumike sehemu yoyote kuanzia biashara, ngazi ya familia na katika shughuli zetu za kila siku” alisema Waziri Mulamula.


Waziri Mulamula alihitimisha hotuba yake kwa kuwapongeza waanzilishi wa Women in Diplomacy pamoja na washiriki kwa kuwa ni jukwaa muhimu la kujifunza na kubadilishana uzoefu na wadau mbalimbali katika eneo la Diplomasia na Uongozi. 

  • Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifurahia jambo wakati akizungumza na Balozi Gertrude Mongela kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Women in Diplomacy
  • Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Waandaaji na Wagini waalikwa kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Women in Diplomacy uliofanyika jijini Dar es Salaam.