Waziri Mahiga aongoza kikao cha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti ya Wizara
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga leo ameongoza kikao cha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti ya Wizara.Hotuba hiyo inatarajiwa kuwasilishwa Bungeni hapo kesho tarehe 29 Mei, 2017.
Kikao hicho kilichofanyika mjini Dodoma katika ukumbi mikutano wa jengo la Hazina pia kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt Susan Kolimba, Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz Mlima Wakurugenzi ,Wakuu wa Vitengo na baadhi ya Maafisa wa Wizara.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Naibu Mhe. Dkt. Susan Kolimba wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu Balozi Dkt.Aziz Mlima.
Mhasibu Mkuu wa Wizara Bw.Paul Kabale akichangia jambo wakati wa kikao
Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akichangia jambo wakati wa kikao
Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Bernard Haule (kulia) akichangia jambo wakati wa kikao
Wajumbe wakiwa katika kikao