Waziri Mahiga Akutana na Mjumbe Maalum wa Haki za Binadam wa Australia
Waziri Mahiga katika mazungumzo yake alieleza kuwa Tanzania ipo tayari kushirikiana na Australia katika kuhakikisha inazisimamia na kuziwezesha Taasisi za Haki za Binadamu za hapa nchini na kuhakikisha haki hizo zinasimamiwa kikamilifu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia nafasi yake ya uenyekiti katika Jumuiya hiyo.