Skip to main content
News and Events

Tanzania yapata Mwakilishi wa Heshima Hong Kong na Macao

Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki kwa pamoja na Bibi Annie Suk-Ching Wu wakisaini Mkataba kumwezesha Bibi Wu kuwa Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania huko Hong Kong na Macao. Tukio hilo lilifanyika kwenye Ubalozi wa Tanzania jijini Beijing, China na kushuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda pamoja viongozi wengine ambao wapo nchini China kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC).

  • Balozi Mbelwa na Bibi Wu wakibadilishana mkataba mara baada ya kuusaini
  • Mhe. Waziri Mahiga akitoa hotuba kumpongeza Bibi Wu kwa kukubali kuiwakilisha Tanzania kwenye maeneo hayo na kumtaka kuiwakilisha vema nchi
  • Picha ya pamoja na viongozi na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo