Skip to main content

Tanzania na Uganda zajadili Kuboresha Sekta ya Uchukuzi

Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt Aziz P. Mlima akiwa katika mazungumzo  na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Uganda Mheshimiwa Mhandisi Monica Ntega  mjini Kampala ambapo walizungumzia changamoto na fursa zilizopo kwa nchi mbili kwenye sekta ya uchukuzi, reli na bandari na ushoroba wa kati. Mazungumzo hayo pia yalihidhuriwa na Waziri wa Nchi wa Ujenzi wa Uganda Jenarali Edward Katumba Wamala.