HABARI PICHA MWILI WA HAYATI DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI UKIAGWA JIJINI DODOMA
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Mhe. Felix Tshisekedi akitoa salamu za rambirambi wakati wa mazishi ya kitaifa ya Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa akisaini kitabu cha maombolezo katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma baada ya kuwasili kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa akitoa salamu za rambirambi wakati wa mazishi ya kitaifa ya Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma
Rais wa Muungano wa Visiwa vya Comoro Mhe. Azali Assoumani akisaini kitabu cha maombolezo katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma baada ya kuwasili kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta akisaini kitabu cha maombolezo katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma baada ya kuwasili kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Lazarius Chakwera akipokelewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge wakati alipowasili katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
Baadhi ya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma
Sehemu ya wananchi waliojitokeza katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma wakati wa mazishi ya kitaifa ya Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi akitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma
Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) Dkt. Stergomena Tax akitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma
Mjane wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akitoa heshima za mwisho kwa mume wake hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Lungu akitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma