Ban Ki-moon ashiriki kwenye ufunguzi wa Ubalozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea
Ban Ki-moon ashiriki kwenye ufunguzi wa Ubalozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea
Kibao cha uzinduzi kikifunguliwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania na Jamhuri ya Korea kwa pamoja.
Mheshimiwa Matilda Masuka (kushoto) Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea akiwakaribisha na kuwashukuru wageni waalikwa waliohudhuria kwa wingi kwenye ufunguzi rasmi wa Ofisi za Ubalozi tarehe 31 Januari 2018. Awali Tanzania ilikuwa inawakilishwa nchini humo kutokea Japan. Mheshimiwa Balozi Matilda Masuka aliteuliwa Desemba 3, 2016 na baadaye kuapishwa kuwa Balozi wa kwanza mwenye makazi yake Mji Mkuu wa Seoul, Jamhuri ya Korea. Anayeangalia (kulia) ni mfanyakazi wa Ubalozini Debora Mikwenda.
Mheshimiwa Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mstaafu akihutubia wageni waliofika kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania. Mheshimiwa Ki-moon, ambaye alitambulishwa kama rafiki mkuu wa Tanzania nchini humo, alipongeza Serikali ya Tanzania kwa kufanikiwa kusimika bendera ya Tanzania nchini mwake baada ya miaka 25 ya uhusiano mzuri wa kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi.