Skip to main content
Balozi Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mabalozi Watatu
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Jamhuri ya Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Prof. Ratlan Pardede. Katika mazungumzo hayo, Mhe. Waziri aliisifu Indonesia kwa hatua ya maendeleo iliyofikia katika nyanja mbalimbali ikiwemo sekta ya kilimo na kuelezea matumaini yake kuwa ujio wa Mhe. Balozi utasaidia kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Indonesia yatakayosaidia Tanzania kujifunza kutokana na maendeleo ya Indonesia.