Skip to main content
News and Events

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA CUBA AFANYA MAZUNGUMZO NA MHE. DKT. ASHATU KIJAJI

Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amekutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba, Mhe. Bruno Parrilla kwenye ofisi za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) tarehe 30 Juni 2022 jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo ya viongozi hao yalijikita katika kuimarisha ushirikiano baina ya mataifa yao kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji mathalan, viwanda vya dawa za binadamu, pembejeo na mifugo, tafiti katika masuala ya afya na kujenga uwezo wa upatikaji wa chanjo nchini.

Vilevile, wamejadili juu ya kukuza thamani ya mazao ya kilimo  na kuwawezesha wananchi kufanya kilimo cha biashara katika soko la kimataifa. 

Aidha, Serikali ya Cuba imewekeza nchini katika kiwanda cha viuadudu ambacho kinatarajiwa pia kuzalisha mbolea baada ya kukamilika kwa taratibu za uwekezaji zilizoafikiwa na pande zote mbili.

Kupitia mazungumzo haya Serikali ya Cuba imeridhia kuendelea kutoa msaada wa kiufundi katika sekta za ushirikiano ili ziweze kuwanufaisha wananchi wa Tanzania na Cuba na kujenga mahusiano ya kimkakati baina yao.
 

  • Kutoka kushoto Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Mhe. Valentino Mlowola, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme na mwisho ni Afisa Mambo ya Nje, Bi Salma Rajab wakifuatilia mazungumzo.
  • Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amekutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba, Mhe. Bruno Parrilla kwenye ofisi za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) tarehe 30 Juni 2022 jijini Dar es Salaam.