Skip to main content
News and Events

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA WABUNGE WA EALA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Naibu Waziri Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk leo tarehe 4 Aprili 2022 wamekutana na kufanya mazungumzo na Wabuge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) wa Tanzania yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.


Akizungumza na Wabunge hao Waziri Mulamula amewapongeza kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya kupitia chombo hicho muhimu katika Jumuiya, ya kuhakikisha Jumuiya inaendelea kustawi zaidi. Vilevile, Waziri Mulamula ametoa wito kwa wabunge hao kuendele kuwa wamoja katika kutetea, kufuatilia na kulinda maslahi ya Taifa na Jumuiya kwa ujumla. 


Wabunge hao ambao walifanya ziara ya kikazi Wizarani wameeleza kuridhishwa na ushirikiano wanaoupata kutoka kwa Viongozi na Watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika utekelezaji wa majukumu yao. Aidha,kupitia Wizara wameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwasilisha kwa wakati ada ya unachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 


Ziara hiyo ililenga kubadilishana mawazo na uzoefu baina yao na Viongozi wa Wizara sambamba na kutoa mrejesho wa maendeleo ya masuala mbalimbali muhimu yanayoendelea katika Jumuiya.

  • Mazungumzo yakiendelea