Skip to main content
News and Events

Waziri Mahiga atembelea kiwanja kitakachojengwa Ofisi za Wizara kilichopo Ihumwa Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Bw. Godwin Kunambi alipofika eneo la kiwanja cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lililopo Eneo la Mji wa Serikali la Ihumwa jijini Dodoma kwa ajili ya kuangalia maandalizi ya mwisho kabla ya kuanza  ujenzi wa Ofisi za Wizara unaotarajiwa kuanza hivi karibuni. Katikati ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu,  Bibi Maimuna Tarishi. 

  • Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Bw. Kunambi kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bibi Dorothy Mwanyika (mwenye miwani myeusi) wakimwonesha Mhe. Waziri Mahiga ramani inayoonesha kilipo kiwanja cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
  • Mhe. Waziri akimsikiliza Bibi Tarishi alipokuwa akimweleza jambo kuhusu ramani hiyo
  • Mhe. Waziri Mahiga akiwaeleza jambo Katibu Mkuu,Ofisi ya Waziri Mkuu, Bibi Tarishi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bibi Mwanyika na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Bw. Kunambi alipofika eneo la kiwanja kilichotengwa kwa ajili ya kujenga Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kilichopo Ihumwa.
  • Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Bw. Kunambi akimwonesha Mhe. Waziri Mahiga ukubwa wa eneo la kiwanja cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
  • Mhe. Mahiga akimsikiliza Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Manyama Mapesi akimweleza kuhusu eneo hilo la kiwanja cha Wizara kilichopo Ihumwa. Wengine ni Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki waliofika kwenye kiwanja hicho.