Skip to main content
News and Events

Sudan Kusini Mwanachama Rasmi EAC

Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki akisaini Mkataba wa Kuiwezesha Sudan Kusini kuwa Mwanachama Kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), tukio hilo la kihistoria limefanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Tukio hilo limeshuhudiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndungai, Jaji Mkuu Mhe. Chande Othmani, Mwanasheria Mkuu, Mhe. George Masaju na Waziri wa Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Augustine Mahiga    

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (wa nne kutoka kulia) na Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini, Mhe. Salva Kiir Mayardit (wa nne kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Wakuu wa Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki