Sudan Kusini Mwanachama Rasmi EAC
Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki akisaini Mkataba wa Kuiwezesha Sudan Kusini kuwa Mwanachama Kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), tukio hilo la kihistoria limefanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Tukio hilo limeshuhudiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndungai, Jaji Mkuu Mhe. Chande Othmani, Mwanasheria Mkuu, Mhe. George Masaju na Waziri wa Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Augustine Mahiga