Skip to main content

Mawaziri wa Tanzania na Uganda wajadili Ujenzi wa Bomba la Mafuta

Ujumbe wa Tanzania uliokwenda nchini Uganda kwa ajili ya ya mkutano wa majadiliano ya ujenzi wa Bomba la kusafirisha mafuta ghfi kutoka Uganda hadi Bandari ya Tanga, ujumbe huo kutoka kulia ni Mhe. January Makamba (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira); Mhe. William Lukuvi(Mb), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. Dkt. Medard Kalemani (Mb), Waziri wa Nishati; Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (Mb), Waziri wa Katiba na Sheria na Mhe. Dkt. Aziz Mlima, Balozi wa Tanzania nchini Uganda. 

Mkutano wa Bomba la Mafuta ghafi ulifanyika Kampala Uganda kuanzia tarehe 21 hadi 25 Januari 2019. Mkutano huo ulianza kwa ngazi za Wataalam, Makatibu Wakuu na kuhitimishwa kwa ngazi ya Mawaziri. Mkutano ulienda vizuri na upo katika hatua nzuri ya majadiliano ili kuanza utekelezaji. Pande zote mbili zimekubaliana mambo mbalimbali ya msingi ambayo.yanafungua na kuandaa njia za utekelezaji wa Mradi.