Baraza la Mawaziri la Kisekta la Mazingira na usimamizi wa Maliasili la Afrika Mashariki wafanyika jijini Arusha
Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Mazingira na usimamizi wa Maliasili la Afrika Mashariki umefanyika leo tarehe 01 Novemba 2024 jijini Arusha.
Katika Mkutano huo Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Mhe. Balozi Dkt. Pindi H. Chana; Waziri wa Maliasili na Utalii akiongozana na Viongozi wengine wakiwemo Mhe. Harusi Said; Waziri wa Nchi kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar na Mhe. Dennis L. Londo; Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia Masuala ya Afrika Mashariki.