Ubalozi wa Tanzania nchini India waadhimisha miaka 55 ya Muungano
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akiwahutubia washiriki wa hafla ya kuadhimisha miaka 55 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliyofanyika katika Hoteli ya Leela Palace jijini New Delhi, India tarehe 26 Aprili 2019. Katika hotuba yake, Balozi Luvanda alieleza kuwa, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni wa kihistoria na wa kupigiwa mfano duniani kote. Pia alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na India ambao umedumu kwa miaka 58.