Skip to main content

Dkt. Ndumbaro akutana na Mwakilishi wa UNHCR

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.), amekuatana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la kutetea wakimbizi la Umoja wa Mataifa Tanzania UNHCR, Chansa Kapaya. 

Katika mazungumzo yao Bi. Chansa alitumia fursa hiyo kujitambulisha kwa mara ya kwanza pamoja na Kumpongeza Dkt. Ndumbaro kwa Kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Wizara wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kwa upande wake Dkt. Ndumbaro alimshukuru kwa kuja ofisini kwake na kumwahidi kumpatia ushirikiano wa kutosha wakati wote wautendaji wa majukumu yake akiwa hapa nchini. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

  • Mazungumzo yakiendelea.Mazungumzo yakiendelea.