Skip to main content
News and Events

BALOZI MINDI ASHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA WA WANAWAKE WA AFRIKA KATIKA UONGOZI

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mindi Kasiga ameelezea uzoefu wa Tanzania kuhusu masuala ya usawa wa kijinsia na uongozi wakati akiwasilisha mada katika Mkutano wa Kimataifa wa Wanawake wa Afrika katika Uongozi (African Women in Leadership International Conference) unaoendelea jijini Durban, Afrika Kusini. 

Mkutano huo ambao umepangwa kufanyika kuanzia tarehe 15-16 Septemba 2022, chini ya wenyeji wa kiongozi wa Jimbo la KwaZulu-Natal Bi. Nomusa Dube-Ncube, hufanyika kila mwaka kwa kuwaleta pamoja viongozi wanawake kutoka Bara la Afrika ili kujadili masuala yanayohusu usawa wa kijinsia na uongozi.

 Miongoni mwa waliohuduhuria mkutano huo ni pamoja na viongozi mashuhuri katika siasa, Sekali na makampuni binafsi kutoka nchi ni; Liberia, Nigeria, Tanzania, Cameroon, Rwanda, na  wenyeji Afrika Kusini. Kongamano lijalo linatarajiwa kufanyika Agosti 2023 jijini Arusha, Tanzania

  • Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mindi Kasiga akielezea uzoefu wa Tanzania kuhusu masuala ya usawa wa kijinsia na uongozi katika Mkutano wa Kimataifa wa Wanawake wa Afrika katika Uongozi (African Women in Leadership International Conference) unaoendelea jijini Durban, Afrika Kusini.
  • Mkutano wa Kimataifa wa Wanawake wa Afrika katika Uongozi (African Women in Leadership International Conference) ukiendelea jijini Durban, Afrika Kusini.