Skip to main content
Jobs and Vacancies

Ajira Sekretariati ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC)

Sekretariati ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) imetangaza nafasi mbalimbali 16 za ajira kupitia tangazo lao lililotolewa tarehe 16 Aprili, 2016 Kumb. Na. SADC/2/3/3/3 katika tovuti ya http://www.sadc.int

Hata hivyo, kulingana na utaratibu wa “quota points” kwa ajira za Sekretariati, kila nchi mwanachama ana jumla ya pointi 121 ambapo kwa Tanzania tumebakiza pointi 5 tu. Pointi hizi hazitoshi kwa wananchi wetu kufanya maombi ya aina yoyote ya ajira za Sekretariati kwa kipindi hiki.

Pointi zinazohitajika kwa ajili ya kuomba nafasi ya ajira ni kuanzia pointi 12. Kwa sababu hiyo, Tanzania haimo katika orodha ya nchi wanachama ambao wanakidhi vigezo (eligible) kwa wakati huu.
Tunawaomba Watanzania waendelee kutembelea tovuti ya SADC na tovuti ya Wizara kwa ajili ya kupata taarifa kuhusu fursa zingine zitakazojitokeza.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,
Dar es Salaam, 22 Aprili, 2016.