Skip to main content
News and Events

WAKUU WA NCHI WA AFRIKA MASHARIKI KUFANYAUTEUZI WA VIONGOZI WA JUMUIYA

Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanatarajiwa kufanya uteuzi wa viongozi mbalimbali wa Jamuiya katika Mkutano wa Kilele wa Wakuu wa Nchi hao unaotarajiwa kufanyika Jumamosi tarehe 27 Februari, 2021. Viongozi waonatarajiwa kuteuliwa ni wale wa ngazi za maaumuzi katika Jumuiya ambao ni Mwenyekiti wa Jumuiya, Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya na Katibu Mkuu wa Jumuiya.

Haya yameelezwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) muda mfupi baada ya hitimisha Mkutano wa 40 wa Kawaida wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki. Mkutano huu uliofanyika kwa njia ya ana kwa ana na video umefanyika katika ngazi tatu, ambazo ni; ngazi ya Wataalam (tarehe 22-23 Februari), ngazi ya Makatibu Wakuu (tarehe 24 Februari) na hatimaye ngazi ya Mawaziri tarehe 25 Februari 2021. 

Waziri Kabudi aliendelea kueleza kuwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri limepitia nyaraka mbalimbali zinazohusu maendeleo na utendaji wa Taasisi mbalimbali za Jumuiya ambapo wamebaini kuwa, licha ya kuwepo kwa changamoto za Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu (COVID-19) Jumuiya pamoja na Taasisi zake zimeendelea kufanya kazi zake kwa ufanisi.

  Kila mwaka, Baraza la Mawaziri la Afrika Mashariki hukutana mara mbili, mkutano mmoja hufanyika mara moja kabla ya mkutano wa Wakuu wa Wakuu wa Nchi. Mikutano ya baraza husaidia kudumisha uhusiano kati ya maamuzi ya kisiasa yaliyochukuliwa kwenye Mkutano na utendaji wa kila siku wa Jumuiya. Kanuni, maagizo na maamuzi yaliyochukuliwa au kutolewa na Baraza yanatekelezwa na Nchi Wanachama na Taasisi zingine zote za Jumuiya isipokuwa Wakuu wa Nchi, Mahakama na Bunge.

Downloads File: