Skip to main content

Dkt. Ndumbaro akutana na Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro aliwasilisha taarifa mbili katika kikao hicho. Taarifa ya kwanza ilihusu hatua zinazochukuliwa na Wizara katika mapambano dhidi ya Ukimwi na taarifa ya pili ilihusu namna Wizara inavyoshirikiana na mashirika ya kimataifa, kikanda na nchi mbalimbali katika kukabiliana na biashara haramu ya dawa za kulevya.